Pakua sasa Bandarini SACCOS App  ufurahie huduma zetu kupitia simu yako ya kiganjani

TANGAZO LA MKUTANO MKUU WA 54 UTAKAOFANYIKA TAREHE 30 OKTOBA 2022

TANGAZO LA MKUTANO MKUU WA 54 UTAKAOFANYIKA TAREHE 30 OKTOBA 2022

Bodi ya Uongozi inawatangazia wanachama wote ambao ni wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama,kwamba Mkutano Mkuu wa 54 kwa Mwaka 2022 utafanyika Dar es salaam tarehe 30 Oktoba 2022 katika ukumbi wa mikutano uliopo Jengo la Bandari (One stop Centre) ghorofa ya nne, jijini Dar es salaam kuanzia saa 02:00 asubuhi.

ZIFUATAZO NI AGENDA ZA MKUTANO MKUU WA 54:

  1. Kufungua Mkutano
  2. Kuthibitisha akidi
  3. Kuchagua Mwenyekiti wa Mkutano
  4. Kupokea na kuthibitisha agenda za Mkutano
  5. Kusoma na kuthibitisha Muhtasari wa Mkutano Mkuu wa mwaka wa 53
  6. Yatokanayo na Muhtasari wa Mkutano Mkuu wa mwaka wa 53
  7. Kupokea na kuthibitisha wanachama wapya na wanaotoka
  8. Kupokea Taarifa ya Mwenyekiti wa Bodi ya Uongozi
  9. Kupokea Taarifa ya Kamati ya Usimamizi
  10. Kupokea na kuthibitisha Taarifa ya Ukaguzi wa Hesabu za mwaka 2021
  11. Kupokea na kuthibitisha Makisio ya Mapato na Matumizi ya mwaka 2023
  12. Uchaguzi wa nafasi wazi ya Mjumbe wa Bodi
  13. Mengineyo
  14. Kufunga Mkutano

Ninawatakia wajumbe wote maandalizi mema na ushiriki mzuri wa Mkutano huo pamoja na mwisho wa mwaka wenye Amani.

TANGAZO HILI LIMETOLEWA NA UONGOZI WA BANDARINI SACCOS


Post a Comment

Translate »