Pakua sasa Bandarini SACCOS App  ufurahie huduma zetu kupitia simu yako ya kiganjani

KUHUSU CHAMA CHETU

Historia Fupi

Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Wafanyakazi wa Shirika la Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania, ulianzishwa rasmi na kusajiliwa katika Daftari la Serikali tarehe 1/8/1968 Mkoani Dar es salaam. Ushirika huu Ulisajiliwa chini ya sheria ya Vyama vya Ushirika ya Mwaka 1968. Makao Makuu yake yapo wilayani Temeke katika Jengo la Bandarini SACCOS lililopo mkabala na Uwanja wa Benjamin William Mkapa. Hati yake ya Usajili katika daftari la Serikali ni DRS.1861. Kufuatana na mabadiliko ya mara kwa mara ya sheria ya Vyama vya Ushirika, hivi sasa Chama kinafanya kazi zake chini ya sheria ya Vyama vya Ushirika Na. 6 ya Mwaka 2013 na Kanuni za SACCOS za Mwaka 2015, Sheria za Huduma Ndogo za Kifedha za Mwaka 2018 na Kanuni za SACCOS za Mwaka 2019 pamoja na Masharti ya toleo la mwaka 2020.

1
2
3

DIRA

Kuwa SACCOS Kiongozi Barani Afrika inayotoa Huduma na Bidhaa Bora za Kifedha kwa Wanachama.

DHAMIRA

Kutoa Huduma Endelevu zinazoendana na Mahitaji Halisi ya Wanachama kwa Teknolojia za Kisasa.

IMANI NA MISINGI YA CHAMA

Ushirikiano, Ubunifu, Ufanisi na Weledi.

Translate »