Pakua sasa Bandarini SACCOS App  ufurahie huduma zetu kupitia simu yako ya kiganjani

UANACHAMA

Kwa mujibu wa Msingi wa kwanza (1) wa Ushirika kimataifa na Masharti ya chama ibara ya 10, Uanachama wa Bandarini SACCOS uko wazi kwa mtumishi yeyote yule wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania au Makampuni mengine yanayofanya kazi Bandarini ili mradi tu awe tayari kufaidika na huduma zake na kufuata Sheria, Kanuni, na Masharti ya Bandarini SACCOS limited. Wanachama ni wale wote waliokuwepo tokea kuanzishwa kwake na wanaoendelea kujiunga kwa mujibu wa masharti ya Chama

SIFA ZA KUJIUNGA BANDARINI SACCOS

  1. Awe mwenye umri wa Miaka isiyopungua 18.
  2. Awe mwenye tabia nzuri, mwaminifu na mwenye akili timamu
  3. Awe amelipa Kiingilio, kununua Hisa za uanachama na kuweka Akiba kwa kiasi kilichowekwa kwa mujibu wa Masharti yaliyopo na awe tayari kushiriki kikamilifu katika shughuli za Bandarini SACCOS Limited.
  4. Awe anaelewa na kuwa tayari kutekeleza madhumuni ya chama kama yalivyoainishwa kwenye Masharti yake na kufafanuliwa katika nyaraka mbalimbali za Chama.
  5. Awe tayari kufuata Masharti ya Chama, Kanuni na sheria za Vyama vya Ushirika wakati wote.
  6. Asiwe na shughuli yeyote ile inayofanana na kuweka au kukopesha wanachama ili kuondoa mgongano wa masilahi.

FAIDA ZA KUJIUNGA NA BANDARINI SACCOS LTD

Katika ubunifu wa mazao ya bidhaa za kifedha na Huduma  kwa wanachama na wadau wa Bandarini SACCOS wanafaidika na;

  1. Viwango shindani na nafuu vya gharama za riba za Mikopo.
  2. Viwango vya pato kwa wanachama waliowekeza fedha zao kwa njia ya Akiba, Amana na Akiba maalum ni vya kuvutia
  3. Wigo mpana wa uchaguzi wa Bidhaa za kifedha (Mikopo)
  4. Hakuna usiri wa gharama wakati wa kafanya Miamala ya uchukuaji Amana na Akiba maalum
  5. Malipo ya gawio kwa wana Hisa na Riba kwenye Akiba na Amana.
  6. Kinga za Majanga ya Mikopo
  7. Fursa ya majadiliano na wateja kuhusu uwekezaji wa fedha zao.

WAJIBU WA MWANACHAMA WA BANDARINI SACCOS

  1. Kukamilisha kununua hisa na kuweka akiba kwa kuzingatia
    Masharti sera na miongozo iliyopo katika chama.
  2. Kufuata na kutekeleza Sera, Sheria na Kanuni za Vyama vya Ushirika, Masharti ya Chama, maazimio ya
    Mikutano mikuu na maelekezo mengine halali kwa mujibu wa Sheria za nchi;
  3. Kurejesha mkopo kwa kufuata mkataba wa mkopo;
  4. Kutoa michango mbalimbali katika kuendeleza madhumuni ya chama kadri itakavyoamuliwa na Mkutano Mkuu;
  5. Kubeba dhamana endapo janga lolote litakipata chama;
  6. Kuwa mwaminifu na kuonesha ushirikiano katika kutekeleza shughuli za chama;
  7. Kumdhamini mkopo mwanachama mwenzake isipokuwa mwanachama aliyedhamini hatakuwa na haki yakudhaminiwa na mwanachama aliyemdhamini katika kipindi kile kile;
  8. Kuhudhuria semina na mafunzo yanayotolewa na Bandarini SACCOS katika mpango wake wa elimu na mafunzo mengine yatakayotolewa na Tume ya Maendeleo ya Ushirika au wadau wa kisekta.

HAKI ZA MWANACHAMA WA BANDARINI SACCOS LTD

  1. Kushiriki kikamilifu katika shughuli za Chama ikiwa ni pamoja na kuhudhuria mikutano yote inayohusika;
  2. Kushiriki katika kutoa uamuzi wa mambo mbalimbali katika Mikutano Mikuu;
  3. Kupiga kura chini ya misingi ya mtu mmoja kura moja bila kujali idadi ya Hisa anazomiliki;
  4. Kuchagua na/au kuchaguliwa katika Uongozi wa chama.
  5. Kuwa na haki sawa kuhusu mali ya Chama na kudhibiti ipasavyo matumizi yake;
  6. Kupatiwa huduma zozote zinazotolewa na chama ilimradi amekidhi masharti yanayoambatana na huduma hiyo;
  7. Kupatiwa taarifa mbalimbali za utekelezaji wa shughuli za Bandarini SACCOS, muhtasari wa mkutano na nyaraka nyingine za chama kwa ajili ya mapitio akiwa katika ofisi za chama;
  8. Kuteua Mrithi;
  9. Kupokea gawio na faida nyingine kutoka katika shughuli za chama kwa kuzingatia masharti; na
  10. Kupewa kitabu cha Akiba au kifaa kingine chenye makusudi hayo.
Translate »