Pakua sasa Bandarini SACCOS App  ufurahie huduma zetu kupitia simu yako ya kiganjani

w

Misingi ya Ushirika

Uwanachama wa hiari na wazi

Uwanachama wa Bandarini SACCOS Limited upo wazi kwa mtu yeyote mwenye sifa na kukidhi vigezo vya kuwa Mwanachama kwa mujibu wa Masharti yake ibara Na. 10 na yuko tayari kufuata Masharti na kufaidika na huduma zake.

Uongozi wa Kidemokrasia

Bandarini SACCOS limited inatawaliwa na Wanachama wenyewe ambao kupitia Bodi yao ya Uongozi imejiwekea sera, Miongozo na maamuzi mbalimbali ya kuendesha Chama. Haya yote hutekelezwa kwa kupitia vikao na Mikutano kwa mujibu wa kanuni na Masharti yaliyopo. Unatambua uwepo wa utawala wa pamoja na kuheshimu maamuzi ya kauli za wengi na sio uwezo wa kifedha alionao Mwanachama katika chama au dhamana yake ya uongozi kutokana na cheo alichonacho.

Ushiriki wa Wanachama katika shughuli za Kiuchumi

Wakati wote chama kitashirikisha wanachama kujenga Mtaji wake wa Msingi kwa uwiano ulio wa usawa utokanao na Hisa zao za uanachama kumiliki Mali za chama kwa pamoja. Aidha itaendelea kuhamasisha wanachama kushiriki katika shughuli za kiuchumi ili kila mmoja aweze kushiriki katika uzalishaji wa ziada ya chama na kugawana ziada hiyo kutokana na ushiriki wa kila mmoja kwa kuzingatia Sheria na miongozo ya kiushirika pamoja na Masharti yake. Sehemu ya Mtaji wake utamilikiwa kwa pamoja na wanachama wote huu ni Mtaji wa Kitaasisi. Unaotokana na mgawanyo wa matengo ya ziada ya kisheria kila mwaka, ruzuku za serikali au misaada ya wahisani. Mtaji wake msingi utaendelea kumilikiwa na mwanachama mmoja mmoja kupitia idadai ya hisa alizonazo zitakazoainishwa kwenye Hati yake ya utambuzi

Kujitawala na Kujitegemea

Bandarini SACCOS limited ni Asasi huru ya kifedha yenye kujitegemea yenyewe kutokana na kuheshimu falsafa ya ushirika ya kujisaidia yenyewe (People helping people) kutoa huduma zake na ikibidi kuingia Mikataba na Serikali, Asasi au watu binafsi kwa ajili ya kuwezeshwa itafanya hivyo ikibidi lakini Wanachama watakuwa na sauti ya mwisho juu ya maamuzi hayo bila kuathiri uhuru na demokrasia yao ya kujitawala

Elimu ya Ushirika

Bandarini SACCOS limited wakati wote, itatilia maanani na kutoa uzito unaostahili katika suala zima la elimu ya ushirika kwa kupanga miongoni mwa shughuli zake za kila siku program za elimu na mafunzo ya ushirika, kupasha habari za shughuli zake katika makundi ya kijamii na yale ya kiuchumi katika maeneo yake ya kikazi. Elimu ya Ushirika inakusudia kuleta uamsho wa kimaendeleo kwa watu wengine na waliokuwemo kwenye Halmashauri ya wilaya Temeke na Halmashauri nyingine zenye maziwa makuu yenye ofisi za Mamlka ya Bandari Tanzania ili hapo baadaye kupata wanachama wapya kujiunga kwa kutambua fursa za kujiendeleza zilizomo kwenye Chama.

Ushirikiano miongoni mwa vyama vya Ushirika

Kwa kuzingatia msingi huu wa kimataifa Bandarini SACCOS limited itaendelea kuhamasisha wanajamii wenye kumiliki biashara na wajasiriamali kujiunga na Chama na kushiriki katika mitandao mingine ya kiushirika yenye manufaa. Chama kitaendelea kudumisha mahusiano ya kindugu na Asasi nyingine za kiushirika kisekta au bila sekta kitaifa na kimataifa kwa lengo la kuendeleza ushirika hapa nchini.

Kujali Jamii

Chama hiki ni Ushirika uliojengwa na wanachama wao ambao waliowengi ni wakazi katika Halamashauri zote za wilaya katika Mkoa wa DSM na Mikoa mingine yenya maziwa makuu na ofisi za mamlaka ya Bandari Tanzania. Kwa ujumla wao ni Waajiriwa na miongoni mwao hujishughulisha na shughuli ndogondogo za Kilimo, Usindakaji, Ufugaji na Biashara.  Sera na mikakati ya utekelezaji wa shughuli za Chama hupitishwa na wanachama kupitia vikao vya Uongozi na Mikutano mikuu ya Wanachama na wajumbe wawakilishi.  Sehemu ya matokeo yake ya kiuchumi yataelekezwa katika kuzisaidia jamii kwa kufanya mawekezo katika nyanja za Kielimu, Afya, Mazingira na shughuli za kiuchumi kupanua wigo wa kimaendeleo kama Mkakati wa kupunguza pengo la umasikini miongoni mwa jamii za kitanzania.

Translate »